Ben Ali akutwa na hatia
Bw Ben Ali na mkewe
Alihukumiwa kifungo cha miaka 15 jela, licha ya kutokuwepo mahakamani.
Mwezi uliopita Ben Ali na mkewe Leila walihukumiwa kifungo cha miaka 35 jela kwa ubadhirifu na matumizi mabaya ya fedha za serikali.
Alikimbilia Saudi Arabia mwezi Januari kufuatia wiki kadhaa za maaandamano- kiongozi wa kwanza kutolewa katika " Ghasia za nchi za kiarabu".
Mpaka sasa Saudi Arabia imeshindwa kumsafirisha Ben Ali, licha ya kuombwa na serikali ya mpito ya Tunisia.
Huko mahakamani, wakili wake, Hosni Beji, alielezea mashtaka ya dawa za kulevya na kuhodhi silaha kama "isiyo na mantiki".
No comments:
Post a Comment