Friday, 6 December 2013

Lissu: Muswada wa kura za maoni ni kinyume cha Katiba

                                                                                                                                                                                                        Dodoma.Kambi ya Rasmi ya Upinzani Bungeni imetaka Muswada wa Kura ya Maoni uondolewe bungeni hadi hapo Bunge litakapofanya marekebisho ya Katiba ya sasa ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwa unapingana nayo.
Awali, muswada huo ulikuwa ujadiliwe katika Mkutano wa 12 wa Bunge lakini uliahirishwa kutokana na wajumbe wa Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala ya Bunge wanaotoka Zanzibar kupinga vikali kura ya maoni kupigwa visiwani humo kwa kuwa tayari huko kuna sheria hiyo.
Akiwasilisha maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni jana, Waziri Kivuli wa Katiba na Sheria, Tundu Lissu alisema katika Katiba ya sasa, hakuna mahali ambako kura ya maoni inatajwa.
Lissu ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki alisema tofauti na Katiba ya Jamhuri, Katiba ya Zanzibar imetambua kura ya maoni kwa kuitaja rasmi katika Katiba na kuiwekea utaratibu.
“Kwa maoni ya kambi ya upinzani, Serikali ya CCM inaogopa kufungua mjadala wa marekebisho ya Katiba ili kuruhusu kura ya maoni kwa hofu kuwa mjadala huo, utapanuliwa kwa kuhoji uhuru wa Tume ya Uchaguzi katika kuendesha na kusimamia uchaguzi,” alisema.
Alisema hofu ya CCM haiwezi kukubaliwa na Bunge kama sababu ya msingi ya kutunga sheria ambazo zinapingana na Katiba.
“Kwani kwa kufanya hivyo itakuwa sawa na kubariki ukiukwaji wa Katiba ambao wabunge wote tuliopo ndani ya ukumbi huu tuliapa kuhifadhi, kuilinda na kuitetea,” alisema Lissu ambaye pia ni Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani bungeni.
Awali, akiwasilisha muswada huo bungeni kwa niaba ya Waziri Mkuu, Waziri wa Nchi (Ofisi ya Waziri Mkuu), Sera, Uratibu na Bunge, William Lukuvi alisema: “Ili kuepuka mkanganyiko unaojitokeza iwapo sheria za uchaguzi zilizopo zitatumika kusimamia uendeshaji wa kura ya maoni, Serikali imeona umuhimu wa kutumia kura ya maoni kwenye mchakato wa kutunga Katiba Mpya.
“Sheria hii si ya kudumu na itafikia ukomo wake, mara tu baada ya Katiba Mpya kupatikana na haya ndiyo madhumuni makuu ya kupendekeza kutungwa kwa sheria hii ya kura ya maoni,” alisema.
Alisema mpigakura aliyesajiliwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura la Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), au Daftari la Kudumu la Wapiga Kura la Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), atakuwa na haki ya kupiga kura ya maoni.
Kamati
Kwa upande wake, Kamati ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala, imeshauri muda wa kukata rufaa kuongezwa hadi siku saba badala ya tano zilizopendekezwa katika muswada huo. Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Pindi Chana alisema Ibara ya 45 ya muswada huo, inaweka masharti kwa kamati ya kura ya maoni ambayo haikuridhika na uamuzi wa mahakama ya chini, kuwasilisha rufaa yake ndani ya siku tano tangu tarehe iliyopata nakala ya hukumu.
Kamati hiyo pia imeshauri Daftari la Kudumu la Wapiga Kura lianze kuboreshwa kwa sababu vijana wengi wamefikisha umri wa kupiga kura na hawajaandikishwa.
Chana alisema kamati inaunga mkono mapendekezo ya muswada huo kuwa kura zitangazwe ndani ya saa 72 tangu kufungwa kwa vituo vya kupigia kura.
“Kamati inashauri Serikali kuandaa vifaa vya kisasa na kuwajengea uwezo watendaji wa tume zote mbili ili waweze kumudu usimamizi wa mchakato wa upigaji wa kura ya maoni kwa weledi na umahiri wa hali ya juu,” alisema. Aidha, alisema kamati inaunga mkono mapendekezo ya muswada huo kuwa matokeo ya kura ya maoni yataamuliwa kwa kigezo cha asilimia 50 ya kura halali zilizopigwa za kuunga mkono swali la kura ya maoni kwa pande zote mbili za Muungano.
“Ibara ya 34(2) inaweka sharti la wingi wa kura halali zilizopigwa katika suala la kura ya maoni kuwa ndilo litakaloamua kuhusu kukubalika au kutokukubalika kwa katiba inayopendekezwa. Kamati inaunga mkono masharti haya kwa kuwa uamuzi wa wananchi ndiyo wa mwisho kuhusu jambo kubwa na nyeti kama la Katiba,” alisema Chana.
Wabunge Z’bar wapinga
Utaratibu wa kuwatumia masheha katika uandikishaji wa vitambulisho vya ukaazi Zanzibar umezua mjadala mkali bungeni baada ya wabunge wa CUF, kupinga kutumika katika kuwapata wapiga kura wa Katiba Mpya.
Akichangia Muswada wa Sheria ya Kura ya Maoni wa mwaka 2013, Mbunge wa Chakechake, Mussa Haji Kombo alitaka kufutwa kwa kipengele kinachotaka kutumika kwa Daftari la Wapiga Kura la Zanzibar katika kupiga kura za maoni kwa kuwa kitawanyima haki Watanzania ambao hawakuandikishwa kutokana na kunyimwa vitambulisho vya ukaazi na masheha.
“Msitugawe kwa kutubagua, leo hii mtu anayeandikishwa Tabora (katika daftari la wapiga kura) haulizwi kitambulisho cha ukaazi lakini wa Micheweni haandikishwi bila kuwa na kitambulisho cha ukaazi,” alisema. “Kuna danadana nyingi katika uandikishaji wa vitambulisho vya ukaazi lakini watoto wa miaka 12 wa wanachama wa CCM wameshapata vitambulisho… zoezi hili ni muhimu tutaliharibu kwa kufuata matakwa ya vyama,” alisema Riziki Omary Juma (Viti Maalumu).
Mbunge wa Mkoani, Ally Khamis Seif, alishauri kuanzishwa kwa daftari lingine la wapiga kura ambalo halitahusisha masharti ya kuwa na vitambulisho vya ukaazi ili kuwapa nafasi Wazanzibari wote kupiga kura katika mchakato huo.
“Kama mimi Sheha wangu wa Konde alininyima kitambulisho cha ukaazi kama ya Mbunge yamekuwa hayo je, Watanzania wa kawaida? Hili jambo litatuletea taabu katika maamuzi haya magumu tunayoyafanya, tuache kutumia daftari la wapiga kura la Zanzibar lile si daftari lile ni uchochezi litatuletea taabu,” aliongeza Mbunge wa Konde, Khatibu Said Haji.
Mwananchi
 Nelson Mandela dies at 95
 
 









Former South African President Nelson Mandela died peacefully at his Johannesburg home on Thursday after a prolonged lung infection. He was 95.
Mandela, the country's first black president and anti-apartheid icon, emerged from 27 years in apartheid prisons to help guide South Africa out of bloodshed and turmoil to democracy. 

"Fellow South Africans, our beloved Nelson Rohlihlahla Mandela, the founding president of our democratic nation, has departed," President Jacob Zuma said in a nationally televised address.

"Our people have lost a father. Although we knew this day was going to come, nothing can diminish our sense of a profound and enduring loss. His tireless struggle for freedom earned him the respect of the world. His humility, passion and humanity, earned him their love," he added. 

Mandela would receive a full state funeral, 

Zuma said, ordering flags to be flown at half mast.

Al Jazeera's Tania Page, reporting from outside Mandela's home in Johannesburg, said that there was a real sense of celebration in tribute to Mandela there, while world leaders were also delivering their tributes. 

People are "singing songs decicated to Mandela", said our correspondent. 


Mandela rose from rural obscurity to challenge the might of white minority apartheid government - a struggle that gave the 20th century one of its most respected and loved figures.

He was among the first to advocate armed resistance to apartheid in 1960, but was quick to preach reconciliation and forgiveness when the country's white minority began easing its grip on power 30 years later.

Mandela was elected president in landmark all-race elections in 1994 and retired in 1999.

He was awarded the Nobel Peace Prize in 1993, an honour he shared with FW de Klerk, the white Afrikaner leader who released from jail arguably the world's most famous political prisoner.

As president, Mandela faced the monumental task of forging a new nation from the deep racial injustices left over from the apartheid era, making reconciliation the theme of his time in office.

The hallmark of Mandela's mission was the Truth and Reconciliation Commission which probed apartheid crimes on both sides of the struggle and tried to heal the country's wounds. It also provided a model for other countries torn by civil strife.

In 1999, Mandela handed over power to younger leaders better equipped to manage a modern economy - a rare voluntary departure from power cited as an example to African leaders.

In retirement, he shifted his energies to battling South Africa's AIDS crisis and the struggle became personal when he lost his only surviving son to the disease in 2005.

Mandela's last major appearance on the global stage came in 2010 when he attended the championship match of the soccer World Cup, where he received a thunderous ovation from the 90,000 at the stadium in Soweto, the neighbourhood in which he cut his teeth as a resistance leader.

Charged with capital offences in the infamous 1963 Rivonia Trial, his statement from the dock was his political testimony.

"During my lifetime I have dedicated myself to this struggle of the African people. I have fought against white domination, and I have fought against black domination."



HISTORIA YA MADIBA

Wednesday, 4 December 2013

Tuesday, 3 December 2013

RAIS DKT. KIKWETE AMTEUA DR. ASHA ROSE MIGIRO KUWA MBUNGE

asha-rose-migiro
THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
 
Telephone: 255-22-2114512, 2116898
              press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425

 
PRESIDENT’S OFFICE,
      THE STATE HOUSE,
              P.O. BOX 9120,  
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Dr. Asha-Rose Migiro kuwa Mbunge.
Taarifa iliyotolewa Ikulu, Dar Es Salaam leo, Jumanne, Desemba 3, 2013, na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, Dr. Florens Turuka inasema kuwa uteuzi huo umeanza jana, Desemba 2, 2013.
Dr. Asha-Rose Migiro ni Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa katika Chama cha Mapinduzi.
 
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
3 Desemba, 2013 

Friday, 29 November 2013

Rais Dkt. Shein Azungumza na Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais

IMG_3289
 
Baadhi ya Viongozi mbali mbali wa Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais,wakiwa katika cha  kujadili utekelezaji wa Mpango kazi wa Wizara hiyo,wa mwaka wa fedha 2013-2014 na robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2013-2014,chini ya Mwenyekiti wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi DK.Ali Mohamed Shein,(hayupo pichani) katika Ukumbi wa Mikutano Ikulu Mjini Zanzibar.
 
IMG_3291
 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi DK.Ali Mohamed Shein,(wa pili kulia) akizungumza na Uongozi wa Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais,katika kikao cha kujadili utekelezaji wa Mpango kazi wa Wizara hiyo,wa mwaka wa fedha 2013-2014 na robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2013-2014,katika Ukumbi wa Mikutano Ikulu Mjini Zanzibar,(kulia) Makamo wa Kwanza wa Rais Maalim Seif Sharif Hamad,(kulia) Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Kwanza  wa Rais Fatma Abdulhabib Fereji,(kusho) na Katibu Mkuu  Kiongozi DSk.Abdulhamid Yahaya Mzee .

Friday, 8 November 2013

JK Ahutubia Taifa kupitia Bunge la Jamhuri ya Muungano mjini Dodoma





Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akilihutubia Taifa kupitia Bunge mjini Dodoma Novemba 7, 2013.

K


Thursday, 31 October 2013

SOMA KWA MAKINI SOMO MUHIMU KUTOKA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI:ASIYE RAIA WA TANZANIA NI NANI?
 
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
 WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
Maswali mengi yanaulizwa kuhusu uraia, hasa wakati huu ambapo zoezi la kuwabaini wageni wanaoishi nchini kinyume cha sheria linaendelea katika maeneo mbalimbali nchini, yakitaka kujua nani hasa ni raia wa Tanzania. 

Kimsingi, masuala ya uraia duniani kote yanaongozwa na falsafa kuu mbili ambazo ni Haki za Kidamu (Jus Sanguinis - The rights of blood), ambapo mtu hupata uraia kutokana na uhusiano wa kidamu na wazazi wenye uraia wa nchi husika. Hii ina maana kwamba, pamoja na mtu kuzaliwa katika nchi husika anatakiwa pia kuwa na mzazi ambaye ni raia wa nchi hiyo. Falsafa hii ndiyo inayofuatwa na nchi ya Tanzania. 

Kwa maana nyingine kuzaliwa pekee nchini Tanzania hakumpi mtu haki ya moja kwa moja ya  kuwa raia wa Tanzania, bali mtu atakuwa raia ikiwa amezaliwa Tanzania na wakati wa kuzaliwa kwake mzazi wake mmoja sharti awe ni raia wa Tanzania.

Falsafa nyingine ni (Jus Soli - The right of Soil), ambayo mtu  hupata Uraia kutokana na kuzaliwa kwake katika ardhi ya nchi fulani. Kufuatana na Falsafa hii, mtu hupata uraia kutokana na kuzaliwa katika nchi husika bila kujali uraia wa wazazi wake.

URAIA WA TANZANIA
Masuala ya uraia nchini Tanzania yanasimamiwa na Sheria ya Uraia ya Tanzania ya mwaka 1995 Sura 357 kama ilivyorejewa mwaka 2002, pamoja na kanuni zake za mwaka 1997. Sheria hii imeanisha aina tatu za uraia wa Tanzania ambazo ni;
1. Uraia wa Tanzania kwa kuzaliwa
2. Uraia wa Tanzania kwa  kurithi
3. Uraia wa Tanzania kwa Tajnisi, au kujiandikisha.

Uraia wa Tanzania wa kuzaliwa:
Utambuzi wa nani ni raia wa Tanzania unazingatia vipindi mbalimbali vya historia ya Tanzania, yaani kabla na baada ya uhuru wa Tanganyika, kabla na baada ya Mapinduzi ya Zanzibar na baada ya Muungano wa Tanzania. Pia, mahali alipozaliwa na alizaliwa na nani kama inavyoainishwa hapa chini:

Aliyezaliwa Tanganyika kabla ya Uhuru

Mtu aliyezaliwa Tanganyika kabla ya Uhuru alitambulika kuwa ni raia wa Tanganyika wa kuzaliwa, ikiwa mmoja wa wazazi wake alizaliwa Tanganyika na anatokana na Raia wa Uingereza, makoloni yake au nchi zilizokuwa chini ya udhamini wa Uingereza

Aliyezaliwa Tanganyika baada ya Uhuru

Mtu aliyezaliwa Tanganyika baada ya Uhuru alitambulika kuwa ni raia wa Tanganyika wa kuzaliwa, ikiwa mmoja wa wazazi wake alikuwa raia wa Tanganyika.

Aliyezaliwa Zanzibar kabla na Baada  ya Mapinduzi

Mtu aliyezaliwa Zanzibar kabla na baada ya Mapinduzi alitambulika kuwa ni raia wa Zanzibar wa kuzaliwa.
Ila, mtu huyo hakutambulika kuwa ni raia wa zanzibar ikiwa wazazi wake walitokana na mataifa yafuatayo; Australia, Ubeligiji, Kanada, Ceylon (Sri Lanka), Ufaransa, Italia, New Zealand, Ureno, Jamhuri ya Ireland, Afrika Kusini na Marekani.

Aliyezaliwa Tanzania siku na baada ya Muungano wa Tanzania
Mtu aliyezaliwa katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania siku na baada ya Muungano, atatambulika kuwa ni raia wa Tanzania wa kuzaliwa ikiwa mmoja wa wazazi wake ni raia wa Tanzania.

Mtu hawezi kuwa raia wa Tanzania kwa kuzaliwa kama wakati wa kuzaliwa kwake hapa nchini, wazazi wake wote hawakuwa raia wa Tanzania; au Baba yake ni Balozi wa nchi ya kigeni na ana kinga ya kibalozi; au mmoja wa mzazi wake alikuwa ni adui wa nchi ya Tanzania (enemy) na mtoto huyo alizaliwa katika eneo lililokuwa likikaliwa na adui.
Sheria ya Uraia ya Tanzania Sura 357 ya mwaka 1995 (R.E, 2002) ndiyo sheria pekee inayotambua sheria zote za nyuma, zilizokuwa zinasimamia masuala yote ya uraia katika vipindi mbalimbali vya historia ya Tanzania.

Kwa mantiki hiyo mtu yeyote ambaye alikuwa raia wa Zanzibar au Tanganyika kwa kuzaliwa, kabla ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar tarehe 25/04/1964, ataendelea kuwa raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  kwa kuzaliwa, mara baada Muungano.
Aidha, mtu yeyote kama hakutambulika kuwa raia wa Zanzibar au Tanganyika kabla ya Muungano, hatatambulika kuwa ni raia wa Tanzania mara baada ya muungano.

URAIA WA TANZANIA KWA KURITHI:
Raia wa Tanzania kwa kurithi ni mtu aliyezaliwa nje ya Tanzania, na anatambuliwa kuwa raia wa Tanzania kutegemeana na kipindi alichozaliwa na uraia wa wazazi wake wakati wa kuzaliwa kwake kama ifuatavyo:

Aliyezaliwa nje ya Tanganyika kabla ya Uhuru

Mtu aliyezaliwa nje ya Tanganyika kabla ya uhuru (akiwa ametokana na raia wa Uingereza na Makoloni yake au himaya ya Mwingereza) alitambuliwa kuwa ni raia wa Tanganyika kwa kurithi endapo baba yake alikuwa raia wa Tanganyika.

Aliyezaliwa nje ya Tanganyika baada ya Uhuru na kabla ya Muungano

Mtu aliyezaliwa nje ya Tanganyika baada ya Uhuru na kabla ya Muungano alitambuliwa kuwa ni raia wa Tanganyika kwa kurithi, ikiwa baba yake alikuwa raia wa Tanganyika.
Sheria ya Uraia ya Tanganyika ya mwaka 1961 haikutoa fursa kwa mama kumrithisha uraia mtoto wake aliyezaliwa nje ya nchi. Hivyo mtu aliyezaliwa nje ya Tanganyika katika vipindi tajwa hapo juu hakutambulika kuwa ni raia wa Tanganyika kwa kurithi kupitia mama yake. 

Aidha, mtu aliyezaliwa nje ya Tanganyika hakutambuliwa kuwa raia wa Tanganyika kwa kurithi iwapo baba yake alikuwa raia wa Tanganyika kwa kurithi. Kwa tafsiri rahisi ni kwamba Raia wa kurithi hawezi kurithisha tena uraia huo kwa mtoto wake aliyezaliwa nje ya Tanganyika.

Aliyezaliwa nje ya Zanzibar kabla ya Muungano wa Tanzania

Mtu aliyezaliwa nje ya Zanzibar kabla ya Muungano atakuwa raia wa Zanzibar kwa kurithi endapo baba yake ni raia wa Zanzibar.
Vile vile, Sheria ya Uraia ya Zanzibar (The Zanzibar Nationality Decree, CAP 39, 1952) haikuruhusu mama raia wa Zanzibar kurithisha uraia kwa mtoto wake aliyezaliwa nje ya Zanzibar. Kwa maana nyingine, mtu aliyezaliwa  nje ya Zanzibar katika kipindi hicho hakutambuliwa kuwa ni raia wa Zanzibar kwa kurithi kupitia kwa mama yake. 

Ieleweke pia kuwa mtu aliyezaliwa nje ya Zanzibar hakutambuliwa kuwa raia wa Zanzibar kwa kurithi ikiwa Baba yake alikuwa raia wa Zanzibar kwa kurithi. Kwa tafsiri rahisi ni kwamba Raia wa Zanzibar kwa kurithi hawezi kurithisha tena uraia huo kwa mtoto wake aliyezaliwa nje ya Zanzibar.

Aliyezaliwa nje ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania siku na baada ya Muungano wa Tanzania

Mtu aliyezaliwa nje ya Tanzania siku na baada ya Muungano atakuwa raia wa Tanzania kwa kurithi endapo mzazi wake mmoja ni raia wa Tanzania kwa kuzaliwa au kuandikishwa/tajnisi.

Ni vyema ieleweke kuwa mtu aliyezaliwa nje ya Tanzania hawezi kuwa raia wa Tanzania kwa kurithi iwapo baba/mama yake ni raia wa Tanzania kwa kurithi. 

Sheria ya Uraia Sura ya 357  ya mwaka 1995 (R.E, 2002) imetoa fursa kwa mama ambaye ni raia wa Tanzania kwa kuzaliwa, tajnisi/kuandikishwa kurithisha uraia wa Tanzania kwa mtoto wake aliyezaliwa nje ya Tanzania.

Aidha, mtu yeyote ambaye alikuwa raia wa Zanzibar au Tanganyika kwa kurithi, kabla ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar tarehe 25/04/1964 ataendelea kuwa raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa namna ile ile mara baada Muungano. 

Mtu yeyote kama hakutambulika kuwa raia wa Zanzibar au Tanganyika kwa kurithi kabla ya Muungano, hatatambulika kuwa raia wa Tanzania kwa kurithi mara baada ya muungano.

Haya yameainishwa katika Sheria ya Uraia ya Tanzania Na.6, 1995 (Sura 357, Rejeo la 2002)  kifungu cha 30.

URAIA WA TANZANIA KWA TAJNISI (NATURALIZATION)

Mtu yoyote ambae siyo raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuzaliwa au kurithi anaweza kuomba uraia wa Tanzania wa tajnisi kwa mujibu wa Sheria ya Uraia Sura 357 ya mwaka 1995, (R.E,2002). 

Kwa mujibu wa sheria hiyo, Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana ya kusimamia masuala ya uraia nchini (Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi), ndiye mwenye mamlaka ya mwisho ya kumpa au kutompa uraia wa Tanzania Mgeni mwenye sifa anayeomba uraia.

Sifa za Kuomba Uraia wa Tajnisi;

Mgeni anaetaka kuomba uraia wa Tanzania anapaswa kuwa na sifa zifuatazo:

(i) Mwombaji awe na umri kuanzia miaka 18 na uwezo wa kufanya maamuzi yanayokubalika kwa mujibu wa sheria za nchi,
(ii) Awe ameishi ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa muda wa miezi 12 mfululizo kabda ya kutuma maombi ya Uraia,
(iii) Katika muda wa miaka kumi kabla ya miezi kumi na mbili hiyo awe ameishi ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kihalali kwa muda usiopungua miaka saba.
(iv) Awe anafahamu vizuri lugha ya Kiswahili au Kiingereza,
(v) Awe na tabia njema,
(vi) Awe na manufaa kwa taifa, yaani awe alichangia na anaendelea kuchangia katika ukuzaji wa uchumi, sayansi na teknolojia na utamaduni wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na
(vii) Awe anakusudia kuishi moja kwa moja ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwa ombi lake la uraia litakubaliwa.

Taratibu za kuomba uraia wa Tajnisi.

Mgeni yeyote mwenye nia ya kuomba uraia wa tajnisi mwenye umri wa miaka 18 na kuendelea anatakiwa kufuata taratibu zifuatazo;
(i) Mwombaji anatakiwa kujaza fomu za maombi ya uraia ambazo zinapatikana katika ofisi zote za Uhamiaji za Wilaya, Mikoa, Afisi kuu ya Uhamiaji Zanzibar na Makao Makuu ya Uhamiaji Dar es Salaam.

(ii) Mwombaji anatakiwa kutoa matangazo ya nia yake ya kuomba Uraia wa Tanzania mara mbili mfululizo kwenye magazeti yaliyosajiliwa Tanzania.

Mchakato wa Kushughulikia Maombi ya Uraia
Ili kuhakikisha kuwa wageni wanaopewa uraia ni wale wenye manufaa kwa Taifa, maombi yote yanapaswa kupitia na kujadiliwa katika vikao vya Kamati za Ulinzi na Usalama za:

Ngazi ya Kata au Shehia (kwa upande wa Zanzibar)
Katika ngazi ya Kata au Shehia anayoishi mwombaji, ambapo atahojiwa na maombi yake kujadiliwa na kikao hicho na hatimaye ombi lake kupelekwa ofisi ya Uhamiaji Wilaya kwa hatua zaidi.

Ngazi ya Wilaya

Katika ngazi hii, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya itajadili maombi ya uraia yaliyowasilishwa kutoka ngazi ya Kata au Shehia, hatimaye maoni na mapendekezo yake hupelekwa katika ngazi ya mkoa.

Ngazi ya Mkoa
Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa nayo itajadili maombi yaliyowasilishwa na kutoa maoni na mapendekezo yake kuhusiana na ombi husika na hatimaye hutumwa kwa Kamishna Mkuu wa Uhamiaji, ambaye atatoa ushauri na mapendekezo yake kwa Mhe. Waziri mwenye dhamana ya masuala ya uraia wa Tanzania kwa maamuzi.

Ombi la Uraia wa Tajnisi kwa Mwanamke aliyeolewa.
Mwanamke mgeni ambaye ameolewa na raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wowote wa uhai wa ndoa yake, anaweza kuwasilisha maombi ya uraia wa Tanzania kwa tajnisi. 

Ombi la uraia kwa mwanamke aliyeolewa linatakiwa kuwasilishwa pamoja na viambatanisho vifuatavyo;

(i)Cheti cha ndoa kilichosajiliwa na Mamlaka husika nchini
(ii) Pasipoti ya taifa lake ambayo haijaisha muda wake
(iii) Kibali cha kuishi nchini ambacho hakijaisha muda wake (Hati ya Mfuasi)
(iv) Vielelezo vinavyothibitisha kuwa mume wake ni raia wa Tanzania.

Ombi la Uraia wa Tajnisi kwa Mtoto
Sheria ya Uraia ya mwaka 1995 Sura 357 (RE 2002), inatoa fursa kwa mzazi au mlezi halali wa mtoto (asiye raia) wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kumuombea mtoto huyo Uraia wa Tanzania. Baada ya maombi rasmi kuwasilishwa, Waziri mwenye dhamana ya uraia anaweza kuruhusu mtoto huyo aweze kupata uraia wa tajnisi.
Waziri mwenye dhamana na masuala ya uraia nchini (Waziri wa Mambo ya Ndani) ndiye mwenye Mamlaka ya mwisho ya kutoa au kutotoa uraia wa Tanzania kwa mwombaji yoyote kwa mujibu wa Sheria ya Uraia ya mwaka 1995 Sura 357, rejeo la 2002.
Makala hii imeandaliwa na
 Timu ya Habari ya Operesheni Kimbunga -
Oktoba, 2013 

Wednesday, 30 October 2013

                          TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

 
THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

 
 
 
Telephone: 255-22-2114512, 2116898
              press@ikulu.go.tz             

 

Fax: 255-22-2113425


 
 
 
 
PRESIDENT’S OFFICE,
      THE STATE HOUSE,
              P.O. BOX 9120,  
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ameondoka nchini jioni ya jana, Jumatatu, Oktoba 28, 2013, kwenda London, Uingereza, kwa ziara ya kikazi ya siku nne ambako atahudhuria Mkutano wa Kimataifa wa Serikali Uwazi (Open Government) uliotishwa na Serikali ya Waziri Mkuu wa Uingereza, Mheshimiwa David Cameroun.

Mkutano huo wa siku mbili utafanyika keshokutwa Jumatano na Alhamisi kwenye Ukumbi wa Queen Elizabeth 2 mjini London.

Miongoni mwa mambo makuu ambayo mkutano huo utazungumzia ni Serikali Uwazi na Ajenda ya Maendeleo Baada ya Mwaka 2015 wakati muongo wa utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo ya Milenia (Millenium Development Goals) unafikia mwisho.

Masuala mengine ambayo yatazungumzwa katika mkutano ambao Rais Kikwete anaambatana na Mawaziri wake watatu ni pamoja na uwazi katika manunuzi ya umma, uwazi katika mikataba, haki ya kupata habari, uwazi katika ukaguzi wa fedha za umma, uwazi wa Serikali na vyombo vya habari, uwazi katika mikataba ya maliasili, uwazi katika maendeleo ya nchi zinazoendelea.

Mawaziri wanaoambatana na Rais Kikwete katika ziara hiyo ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mheshimiwa Bernard Membe, Waziri wa Sheria na Katiba Mheshimiwa Mathias Chikawe na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utawala Bora Serikali ya Mapinduzi, Zanzibar Mheshimiwa Mwinyihaji Makame.

Rais Kikwete anatarajia kurejea nyumbani Jumamosi, Novemba 2, 2013.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.

29 Oktoba, 2013

Monday, 28 October 2013

Takwimu za wapiga kura wapya katika majimbo matano ya Unguja zimepotea.


Chama Cha Wananchi (CUF) kimeanza kumtilia shaka Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Bw. Jecha Salim Jecha na kudai kuwa hana sifa za kuwa Mwenyekiti wa Tume hiyo.
Akizungumza na wanachama na wapenzi wa Chama hicho katika mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Pwepweu Tumbe, Katibu Mkuu Maalim Seif Sharif Hamad amesema Jecha ni mkereketwa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), na kwamba kwa mazingira hayo hatoweza kutenda haki katika uchaguzi.
Akielezea zaidi kuhusu madai hayo Maalim Seif amedai kuwa katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, Jecha aliingia katika mchakato wa kugombania nafasi ya Ubunge katika Jimbo la Kwamtipura kupitia CCM, lakini hakuweza kupata nafasi baada ya kushindwa katika mbio za kugombea nafasi hiyo.
Maalim Seif ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar ameibua hoja hiyo baada ya kuwepo taarifa kuwa takwimu za wapiga kura wapya katika majimbo matano ya Unguja zimepotea kwenye Komputa, na kudai kuwa huo ni mkakati maalum ulioandaliwa na Chama Cha Mapinduzi kwa kushirikiana na Tume ya Uchaguzi Zanzibar.
Ameyataja majimbo yanayodaiwa kupoteza Takwimu zake za wapiga kura wapya kuwa ni Bumbwini, Donge, Kitope, Bububu na Mfenesini.
Maalim Seif ameenda mbali zaidi kwa kumtaka Mwenyekiti huyo ajiuzulu wadhifa huo na kama akishindwa basi Rais wa Zanzibar achukue jukumu la kumfuta kazi.
“Kwa kweli Mwenyekiti huyu hana sifa kabisa za kuwa Mwenyekiti wa ZEC kwa sababu ni mkereketwa wa CCM aliyegombea nafasi ya Ubunge katika uchaguzi mkuu wa 2010, hawezi kabisa kutenda haki katika uchaguzi”, alisema Maalim Seif na kuongeza
“Kwa hivyo namuomba sana Mwenyekiti huyu ajiuzulu, na kama akishindwa basi kwa heshima zote namuomba Rais Dokta Shein amuwajibishe kwa kumfuta kazi”, alisisitiza.
Katika hatua nyengine Maalim Seif amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Rais Jakaya Mrisho Kikwete kwa moyo wake wa kusimamia vyema mchakato wa mabadiliko ya katiba ya Tanzania.
Amesema kitendo cha kukubali kukutana na viongozi wa vyama vya upinzani ni hatua muhimu katika kuendeleza mchakato huo ambao ulionekana kuanza kuzorota baada ya vyama vya upinzani kuukataa muswada wa marekebisho ya sheria ya mabadiliko ya katiba.
Amewasisitiza wananchi wa Zanzibar kuacha tofauti zao katika kipindi hiki cha mchakato wa mabadiliko ya katiba, na badala yake  washirikiane katika kupata katiba iliyo bora, yenye maslahi kwa Zanzibar na vizazi vijavyo.
Mapema akizungumza katika mkutano huo, Mwakilishi wa Tumbe Mhe. Rufai Said Rufai amesema atashirikiana na viongozi wengine wa Jimbo hilo pamoja na wa Wilaya ya Micheweni kuhakikisha kuwa vijana wote waliotimiza umri wa miaka 18 katika jimbo hilo wanapata vitambulisho vya Mzanzibari Mkaazi (ZAN ID).
Katika Mkutano huo Maalim Seif alikabidhi kadi 1536 kwa wanachama wapya waliojiunga na chama hicho wote wakitokea jimbo la Tumbe, ambapo miongoni mwao wametoka Chama Cha Mapinduzi.

Saturday, 26 October 2013

SMZ yaridhishwa na jitihada za UN kuleta maendeleo Zanzibar 


un_flag
 
Wakati Umoja wa Mataifa ukiadhimisha miaka 68 tangu kuasisiwa kwake, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeelezea kuridhishwa na jitihada za Umoja huo katika kuiunga mkono Zanzibar kupitia nyanja tofauti zikiwemo kuwajengea uwezo vijana pamoja na elimu ya afya hasa kwa akina mama na watoto.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad ameeleza hayo katika hafla maalum ya kuadhimisha siku ya Umoja wa Mataifa iliyofanyika hoteli ya Serena Mjini Zanzibar.
Amesema Umoja wa Mataifa umekuwa mstari mbele kuchangia juhudi za maendeleo nchini kupitia mashirika yake yakiwemo Shirika la Mpango wa Maendeleo (UNDP), Shirika la kuhudumia watoto (UNICEF), Shirika la Kazi (ILO) na Shirika la Afya duniani (WHO).
Amesema mafanikio makubwa yamepatikana kutokana na kuwepo kwa mashirika ya Umoja huo, na kwamba Serikali inathamini mchango wa Umoja wa Mataifa katika maendeleo ya nchi.
Amehamisha kuwa Serikali itaendeleza uhusiano mwema uliopo kati yake na Umoja wa Mataifa, na kuahidi kufanya juhudi za makusudi kuona kuwa malengo ya millennium yaliyoanzishwa na Umoja huo yanafikiwa ifikapo mwaka 2015.
Amesema pamoja na mambo mengine Umoja wa Mataifa umekuwa mstari wa mbele katika kuhimiza umoja na mshikamano duniani, sambamba na kusimamia masuala ya amani, utawala bora na haki za binadamu.
Maalim Seif ametaja baadhi ya michango muhimu iliyotolewa na Umoja huo kwa Zanzibar kuwa ni pamoja na kuunga mkono juhudi za vijana hasa wa vijijini katika kukabiliana na tatizo la ajira, kusaidia mpango mkakati wa vijana Zanzibar, elimu, pamoja kusaidia juhudi za serikali katika kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi.
Hata hivyo ameuomba Umoja huo kuongeza misaada yake kwa Zanzibar, hasa katika kuwawezesha vijana kuweza kukabiliana na ukosefu wa ajira na kupunguza umaskini.
Nae Mwakilishi Mkaazi wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania, Alberic Kacou amesema  wanaadhimisha siku hiyo kutathmini hatua zilizofikiwa na Umoja huo katika kutunza amani na maendeleo duniani.
Amesema katika tathmini yake kwa mwaka 2013, Umoja huo unakabiliwa na changamoto ya kiusalama kutokana na mapigano yanayoendelea nchini Syria.
Amesema mamilioni ya watu wamekuwa wakiutegemea Umoja huo kwa misaada ya kibinadamu ikiwa ni pamoja na janga la njaa, na kwamba hautosita kutoa misaada hiyo kwa kadri itavyohijatika katika nchi mbali mbali.
Kuhusu malengo ya millennium, Kacou amezitaka nchi wanachama kuendeleza juhudi ili kuona kuwa zinafikia malengo hayo ifikapo mwaka 2015, huku akilenga zaidi suala la kupunguza umaskini.
Maadhimisho hayo yalihudhuriwa na vingozi mbali mbali wakiwemo mabalozi wadogo waliopo Zanzibar, Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe. Pandu Ameir Kificho na Katibu Mkuu Kiongozi Mhe. Abdulhamid Yahya Mzee.
Hassan Hamad (OMKR)
Oktoba 26, 2013

Serikali ya China yatoa msaada wa fedha kwa SMZ 


Waziri wa Fedha  Omar Yussuf Mzee
Waziri wa Fedha Omar Yussuf Mzee
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imetiliana Saini mkataba wa makubaliano na Serikali ya China  ambapo nchi hiyo itaipatia Zanzibar msaada wa zaidi ya  Dola milioni sita za Marekani ikiwa ni uendelezaji wa misaada inayotolewa na nchi hiyo kwa Zanzibar katika nyanja mbali mbali za Uchumi.
Sherehe za utiaji saini makubaliano hayo  zilifanyika leo  katika Wizara ya Fedha, Vuga  ambapo Waziri wa Wizara hiyo  Omar Yussuf Mzee aliiwakilisha Zanzibar na Balozi mdogo wa China hapa Zanzibar Xie Yunliang aliiwakilisha nchi yake.
Akizungumza baada ya utiaji saini, Waziri wa Fedha alisema kua msaada huo utalenga katika nyanja mbali mbali ikiwemo ujenzi wa Hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani, Uchimbaji wa visima vya maji safi na salama na kupambana na mbu wa malaria  katika maeneo ambayo maradhi hayo bado yapo.
Alisema kazi iliobakia hivi sasa ni kwa Idara ya  Hazina kuwasiliana na wahusika  ili utekelezaji wa makusudio hayo yaweze kufikiwa kwa haraka.
Nae Balozi Xie Yunliang alisema kuwa  Zanzibar na China ni nchi mbili zenye uhusiano mzuri  wa muda mrefu hali ambayo imeifanya kua ni rafiki wa karibu.
Alisema  makubaliano hayo ni muendelezo wa misaada wanayoitowa ili kuona Zanzibar inapiga hatua katika juhudi zake za kukuza Uchumi na Maendeleo ya wananchi.
Utiaji saini makubaliano hayo ulikwenda  sambamba na  kukabidhiwa hati za Taa za Barabarani zinazo tumia nishati ya jua katika Manispaa ya Mji wa Zanzibar ambapo mradi huo ulifadhiliwa na Serikali ya China.

Friday, 25 October 2013

Mageuzi tena Katiba Mpya


Mwandishi Wetu
23 Oct 2013
RASIMU ya awali ya Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo imekwishajadiliwa katika Mabaraza ya Katiba na sasa inafanyiwa uchambuzi na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, inafanyiwa mabadiliko kadhaa ya msingi huku mfumo wa Serikali Tatu ukiendelea kubaki kama ilivyopendekezwa, Raia Mwema limeelezwa.
Kati ya mambo ya msingi ambayo yataingizwa katika awamu ya pili ya rasimu ya Katiba Mpya ikakayowasilishwa kwa Rais na kisha katika Bunge la Katiba mara baada ya kukamilika ni pamoja na mipaka kati ya Tanganyika na Zanzibar, kuongozwa kwa mambo ya Muungano kutoka saba yaliyopendekezwa awali hadi 10, kinga dhidi ya mashitaka ya Rais, majimbo ya ubunge kwa Bunge la Muungano, ulinzi na usalama pamoja na vyama vya siasa kuweza kufukuza wabunge walioshinda kwa ridhaa ya vyama hivyo.
Mipaka ya Tanganyika na Zanzibar
Mipaka ya Tanganyika na Zanzibar ni lazima iwekwe ndani ya Katiba ili kila mamlaka ya nchi washirika iendeshe shughuli zake bila kuingiliana. Uchimbaji wa mafuta au uvuvi wa samaki, Tanganyika ijue iishie wapi na Zanzibar iishie wapi.
Kwa sasa katika rasimu ya Katiba Mpya, sura ya kwanza inayozungumzia mipaka, alama, lugha, utamaduni na tunu za taifa, ibara yake ya pili inaeleza kuhusu eneo la Jamhuri ya Muungano kuwa ni eneo lote la Tanzania Bara ikijumuisha sehemu yake ya bahari na eneo lote la Zanzibar ikijumuisha sehemu yake ya bahari.
Mambo ya Muungano kutoka saba hadi 10
Kwa sasa, katika rasimu ya kwanza ya Katiba mpya, mambo ya Muungano yanatajwa kuwa saba ambayo ni mosi, Katiba na mamlaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; pili, ulinzi na usalama wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; tatu, uraia na uhamiaji; nne, sarafu na benki kuu; tano, mambo ya nje; sita, usajili wa vyama vya siasa na saba; ushuru wa bidhaa na mapato yasiyo ya kodi yatokanayo na mambo ya Muungano.
Katika mambo hayo saba, yatanatarajiwa kuongezwa matatu kwa mujibu wa maoni yaliyotolewa wakati wa Mabaraza ya Katiba. Yanayoweza kuongezwa ni Haki za Binadamu, Tume Huru ya Uchaguzi, Maadili na Miiko ya Uongozi.
Kinga dhidi ya mashitaka ya Rais
Rasimu ya kwanza ya Katiba mpya iliyojadiliwa katika Mabaraza ya Katiba ilipendekeza katika Ibara ya 83(1) na (2) kuhusu kinga dhidi ya mashitaka ya Rais. Katika ibara hiyo ya 83 (1) inaeleza; Wakati Rais akiwa madarakani, hatashitakiwa wala mtu yeyote hataendesha mashtaka ya aina yoyote dhidi yake mahakamani kwa ajili ya kosa lolote la jinai.
Ibara ya 83(2) inaeleza; wakati Rais ameshika madaraka kwa mujibu wa Katiba hii, haitaruhusiwa kufungua mahakamani shauri la madai kuhusu jambo lolote alilolitenda au alilokosa kulitenda yeye binafsi kama raia ama kabla au baada ya kushika madaraka ya Rais, ila tu kama angalau siku thelathini kabla ya shauri kufunguliwa mahakamani, Rais atapewa au ametumiwa taarifa ya madai kwa maandishi kwa kufuata utaratibu uliowekwa kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge, na taarifa hiyo ikiwa inatoa maelekezo kuhusu chanzo cha shauri hilo, kiini cha madai yenyewe, jina lake na anwani ya mahali anapoishi huyo mdai na jambo hasa analodai.
83 (3) inaeleza; isipokuwa kama ataacha kushika madaraka ya Rais kutokana na kura ya kutokuwa na imani na Rais, haitakuwa halali kwa mtu kumshitaki au kufungua mahakamani shauri lolote la jinai au la madai dhidi ya mtu aliyekuwa anashika madaraka ya Rais baada ya kuacha madaraka hayo kutokana na jambo alilofanya wakati alipokuwa bado anashika madaraka ya Rais.
Katika eneo hili kuhusu kinga dhidi ya mashitaka ya Rais, maoni mengi ambayo yanapewa nafasi kubwa kuwekwa katika rasimu ijayo ya Katiba mpya itakayowasilishwa katika Bunge la Katiba ni kutaka kuwapo na mwanya wa kumshitaki Rais baada ya kuondoka madarakani, hasa kwa makosa ambayo atakuwa amefanya yasiyohusiana na madaraka yake ya urais.
“Huwezi kuwa na kinga ya jumla katika kumshitaki Rais ambaye amekwishaondoka madarakani, tunaweza kuwa na kinga ya kutomshitaki kwa mambo ambayo ameyafanya kama Rais na lakini lazima kuwe na nafasi ya kumshitaki kwa mambo ambayo ameyafanya akiwa madarakani ambayo si sehemu ya majukumu ya Rais. Kwa mfano, ikitokea Rais amehusishwa na matukio ya hovyo kama ubakaji. Jiulize, ubakaji ni kazi za Rais…kama siyo kwa nini asishtakiwe baada ya kuondoka madarakani?” kilieleza chanzo chetu cha habari.
Majimbo ya Bunge la Muungano utata
Kwa kuzingatia maoni ya wadau wengi wa Mabaraza ya Katiba, kumekuwa na hali ya kupaki njia panda katika Tume ya Mabadiliko ya Katiba, ambayo katika rasimu yake ya awali ilipendekeza katika Ibara ya 105 (2) kuhusu aina za wabunge ambao ni (a) waliochaguliwa kuwakilisha majimbo ya uchaguzi (b) wabunge watano watakaoteuliwa na Rais kutoka miongoni mwa watu wenye sifa za kuchaguliwa kuwa waunge kuwakilisha watu wenye ulemavu kwa kuzingatia uwiano wa Washirika wa Muungano.
Lakini sehemu inayoiweka njia panda Tume ya Mabadiliko ya Katiba kwa sasa, hasa baada ya kukusanywa kwa maoni ya Mabaraza ya Katiba ni kuhusu muundo wa majimbo ya ubunge, kwa upande wa Tanzania Bara na Zanzibar.
Katika rasimu ya awali, ilipendekezwa katika Ibara ya 105 (3) kwamba;…kila mkoa kwa upande wa Tanzania Bara na wilaya kwa upande wa Zanzibar, itakuwa jimbo la uchaguzi.
Hoja inayoibua utata hapo ni kwamba, kwa sababu, kwa mfano, Rais wa Tanganyika (Tanzania Bara) anaweza kugeuza wilaya kuwa mkoa na kwa hiyo akaweza kuongeza idadi ya majimbo ya ubunge na kwa sababu, Rais wa Zanzibar anaweza kubadilisha shehia kuwa wilaya ili kuwa na idadi kubwa ya majimbo na hatimaye idadi kubwa ya wabunge katika Bunge la Muungano, kwa sababu zozote zile ikiwamo kuwa na idadi kubwa ya wabunge kwa ajili ya kulinda maslahi ya upande anaoongoza, kigezo cha mkoa au wilaya kuwa jimbo la uchaguzi kinapoteza mantiki.
Sasa inaweza kupendekezwa, kuwapo kwa idadi mahsusi ya majimbo ya uchaguzi na hasa kwa kigezo cha idadi ya usawa kati ya Bara na Zanzibar, yaani asilimia 50 ya wabunge wa Bunge la Jamhuri watoke Bara na wengine asilimia 50 ya idadi ya wabunge wa Bunge hilo watoke Zanzibar, bila kujali ukubwa wa nchi hizo Washirika.
Ulinzi na Usalama
Katika rasimu ya sasa, kwa mfano Ibara ya 224, inaeleza; kutakuwa na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ambaye atateuliwa na Rais baada ya kushauriana na Baraza la Ulinzi na Usalama wa Taifa. Baraza hilo la Ulinzi na Usalama wa Taifa linatajwa katika 221(1) kuundwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano; Makamu wa Rais; Rais wa Tanzania Bara; Rais wa Zanzibar; Waziri mwenye dhamana na ulinzi; Waziri mwenye dhamana ya mambo ya ndani ya nchi, Waziri mwenye dhamana na mambo ya nje; Waziri mwenye dhamana na usalama wa taifa; waziri mwenye dhamana ya fedha; Mwanasheria Mkuu wa Serikali; Mkuu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania; Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa na Mkuu wa Jeshi la Polisi la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kutokana na mapendekezo ya Mabaraza ya Katiba, eneo hili linaweza kufanyiwa mabadiliko ili wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama nchini wateuliwe na Rais lakini wathibitishwe na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mfano unaopendekezwa hapa ni kama wa sasa wa namna Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anavyopatikana, ambaye jina huteuliwa na Rais, kisha jina lake kuwasilishwa bungeni kwa ajili ya kupitishwa au hata kukataliwa.
Chama kuweza kufukuza mbunge
Kwenye rasimu ya awali, kuhusu uwajibikaji wa wabunge katika Ibara ya 123(2) na (3) zinagongana kimantiki. Wakati ibara ya 123(2) ikieleza; Mbunge aliyependekezwa na chama cha siasa, hatapoteza ubunge wake ikiwa mbunge huyo atafukuzwa au kuvuliwa uanachama wa chama chake na Ibara ya 123(3) inaeleza; endapo mbunge, kwa ridhaa yake atajiondoa au kujivua uanachama kutoka chama chake cha siasa, mbunge huyo atapoteza sifa za kuwa mbunge na atasita kuwa mbunge.
Kutokana na mgongano huo wa kimantiki, mabadiliko yanatajwa kuweza kufanyika kwamba chama kinapomvua uanachama mbunge husika basi na ubunge wake ukomee hapo. Katika hili, kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari, inaelezwa vyama vyote vikubwa vya siasa nchini vimekubaliana na kuna nafasi kubwa ya kupitishwa.
Eneo jingine ambalo litafanyiwa marekebisho kwa mujibu wa vyanzo vyetu hivyo vya habari ni namna ya kumwondoa mbunge asiyejali maslahi ya wananchi wake kabla ya muda wake wa muhula kuhitimishwa.
Katika rasimu ya awali, ibara ya 124 (1) inaeleza, bila kuathiri masharti ya Ibara ya 123 ya Katiba hii, wananchi watakuwa na haki ya kumwondoa mbunge wao madarakani, endapo mbunge atafanya mojawapo ya yafuatayo; (a) kuunga mkono sera ambazo zinaenda kinyume cha maslahi ya wapiga kura au kinyume cha maslahi ya taifa.
Katika kipengele hiki, uzoefu wa ushindani wa uvunaji, usafirishaji na matumizi ya gesi ya Mtwara unatumika kujenga hoja ya kuondoa kipengele hiki. Chanzo chetu cha habari kinaeleza; “Kwa mfano, Mtwara maslahi ya taifa yanaonyesha gesi hiyo isafirishwe na kuhudumia taifa zima lakini wananchi wa jimbo mojawapo kwa mfano walikuwa wanasema gesi hiyo isisafirishwe, kama mbunge wa jimbo husika atasema isafirishwe maana yake hazingatii maslahi ya wananchi wake kwa hiyo afukuzwe….hii haijakaa sawa.
“Kwa hiyo, kipengele hiki kinaweza kufanyiwa marekebisho bila kupora haki ya wananchi kumwondoa mbunge wao. Kwa mfano, inaweza kuelezwa katika Katiba wananchi wanaweza kumwondoa mbunge wao kwa mujibu wa sheria itakayotungwa na Mbunge,” anaeleza mtoa habari wetu kutoka serikalini.
Mchakato unaendelea
Kwa sasa Tume ya Mabadiliko ya Katiba inayoongozwa na Mwenyekiti wake, Jaji Joseph Warioba ipo katika hatua ya uchambuzi wa maoni yaliyotokana na mikutano ya Mabaraza ya Katiba na baada ya hapo, itaandika rasimu ya Katiba Mpya awamu ya pili ambayo itakabidhiwa kwa Rais ambaye ataitisha Bunge la Katiba kwa ajili ya kujadiliwa na baada ya hapo, rasimu hiyo itawasilishwa kwa wananchi kwa ajili ya kupigiwa kura ya maoni.
Bunge la Katiba linaweza kurekebisha au kuongeza masuala mbalimbali katika rasimu hiyo y awamu ya pili itakayowasilishwa kwao na baada ya kuridhika, na rasimu hiyo kuwasilishwa kwa wananchi kwa ajili ya kupigiwa hizo kura za maoni, wananchi watapiga kura ya maoni kwa njia ya kujibu swali la ndiyo kama wanaikubali au hapana kama hawaitaki rasimu hiyo.
Mchakato wa upigaji na usimamizi wa kura ya maoni utaendeshwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo kwa sasa inaongozwa na Jaji Damian Lubuva.
..- See more at: http://www.raiamwema.co.tz/mageuzi-tena-katiba-mpya#sthash.kX75XLfW.dpuf

Thursday, 24 October 2013

Mapendekezo ya wapinzani mazito

                                                                                                                                                                                                        WAREJESHA MENGI YALIYOKATALIWA NA CCM
Na Josephat Isango
SIKU chache baada ya Rais Jakaya Kikwete, kukutana na viongozi wa vyama vyenye wabunge kuzungumzia upungufu katika muswada wa marekebisho ya sheria ya sheria mabadiliko ya katiba, viongozi wa vyama hivyo wametoa mapendekezo mazito.
Tanzania Daima Jumatano limedokezwa kuwa mapendekezo hayo mengi ni yale yaliyokataliwa na wabunge wa Chama Cha mapinduzi (CCM) wakati wakipitisha muswada huo bungeni.
Mapendekezo hayo ya wapinzani yanaonekana yatazua mtafaruku mkubwa bungeni iwapo serikali itaamua kuyapeleka, hasa baada ya Rais Kikwete kuwataka wapinzani kuandaa mapendekezo ya kina ya upungufu wa sheria hiyo na wayawasilishe haraka iwezekanavyo serikalini ili iunde kamati maalumu ya kujadili upungufu.
Tanzania Daima Jumatano limebaini kuwa viongozi hao wa vyama vya upinzani waliokutana Oktoba, 17, 2013 walijadili na kutoa mapendekezo kadhaa mbayo wameyawasilisha serikalini kama walivyoagizwa na Rais Kikwete.
Mapendekezo
Wapinzani hao wanapendekeza kifungu 22 (2A) cha sheria kama ilivyo sasa kifutwe kabisa, na kwamba wajumbe waliotajwa katika kifungu cha 22 (1) (c) watateuliwa na taasisi watakazowakilisha, na kwamba idadi ya wajumbe hao iongezeke kutoka 166 kwa mujibu wa sheria ya sasa hadi 438.
Wamependekeza kuwa makundi yote yanayostahili kuwakilishwa katika Bunge Maalumu la Katiba yatafafanuliwa na idadi ya wawakilishi wao kuwekwa wazi katika jedwali la pili la sheria.
Pendekezo jingine linataka kuzingatia usawa wa kijinsia, kifungu kidogo (2b) kifutwe na kuandikwa upya “uteuzi wa wajumbe wa Bunge Maalumu chini ya kifungu kidogo (1) ( c ) utazingazia kanuni za sifa na zuoefu wa watu walioteuliwa, na idadi ya wajumbe wanawake haitapungua theluthi moja ya wajumbe walioteuliwa kutoka katika makundi hayo.”
Kwa kuzingatia dhana ya usawa wa wabia sawa wa Muungano bila kujali ukubwa wa kila nchi, idadi ya watu wake na kuzingatia haja ya kujenga muafaka na maridhiano ya kisiasa kuhusu muungano wetu, viongozi wa vyama, wamependekeza kama ilivyokuwa katika uteuzi wa wajumbe wa Tume ya Katiba ya Mabadiliko ya Katiba, kutakuwa na uwakilishi sawa katika Bunge Maalumu kati ya washiriki wa Muungano.
Vile vile wamependekeza kuwa kifungu 22(1) kirekebishwe kwa kuongeza aya ya (d) isomeke “wajumbe wa Bunge Tume ambao hawatakuwa na haki ya kupiga kura katika Bunge Maalumu yaani watakuwa wajumbe kwa nafasi zao ‘ex officio’ kwenye Bunge Maalumu.”
Hivyo kifungu (c) cha zamani za 37 (1) kirejeshwe ili kuwezesha uwepo wa tume hadi baada ya matokeo ya kura ya maoni kutangazwa, na idadi ya wajumbe wa Bunge Maalumu itakuwa 908, kwa mchanganuo wa 357 Bunge la Jamhuri, 81 Baraza la Wawakilishi, na 438 watakaoteuliwa na makundi tajwa katika kifungu 22(1) (c) na wajumbe 32 ‘ex officio’ wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Pia wamependekeza kwamba kifungu 26 (4) na (5) vifutwe badala yake kifungu (3) kirekebishwe ili kuweka wazi kwamba wajumbe wa Bunge Maalumu wataendelea na majadiliano hadi kifungu husika kitakapoungwa mkono na theluthi mbili ya wajumbe wote wa Bunge Maalumu kutoka Tanganyika na idadi hiyo hiyo kutoka Zanzibar.
Mapendekezo hayo pia yamesema kwa jinsi sheria ilivyopitishwa kuzungumzia nafasi ya kuwa Mwenyekiti au Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalumu sifa zake ni lazima mgombea awe na Shahada ya Chuo Kikuu kilichotambulika na uzoefu na ujuzi uliothibitika wa kuongoza mihadhara na mabaraza, kifungu hicho kitakuwa cha kibaguzi miongoni mwa wajumbe wa Bunge Maalumu ambao wengine hawajahitimu vyuo vikuu hivyo kukosa sifa ya kuteuliwa au kuchaguliwa.
Hata hivyo kwa kuwa kifungu hicho hakikutoa tafsiri ya neno mihadhara au mabaraza na mthibitishaji mwenyewe kutotajwa, wamependekeza kuwa mjumbe yeyote wa Bunge Maalumu awe na sifa ya kugombea na kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti au Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalumu, na viongozi hao wachaguliwe badala ya kugombea.
Wapinzani wataka ushirikiano
Wakati Tanzania Daima Jumatano ikidokezwa kuwasilishwa kwa mapendekezo hayo serikalini, viongozi wakuu wa vyama vya CCM, CHADEMA, CUF, NCCR- Mageuzi, TLP na UPDP, wametaka mchakato wa kupata katiba mpya ulenge maslahi mapana ya nchi na wananchi kuliko kufikiria maslahi ya vyama au makundi fulani katika jamii.
Viongozi hao walikutana na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, ambapo Mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia nchini (TCD), James Mbatia alisema kutokana na umuhimu wa upatikanaji wa katiba mpya, vyama vimedhamiria kuhakikisha kuwa mchakato wa katiba unafanyika kulenga maslahi mapana ya nchi.
“Sote kwa pamoja tunatambua tofauti mbalimbali ambazo ziko baina ya vyama vyetu kiitikadi na kimtizamo, lakini tunachukua jukumu kwa nia safi kuhakikisha kuwa Watanzania wanapata katiba wanayoitaka,” alisema.
Vyama hivyo pia kwa tamko la pamoja vimesema vilikubali wito wa Rais Jakaya Kikwete alioutoa kupitia hotuba yake kwa Watanzania Septemba 4 na walipokutana naye Oktoba 5, mwaka huu, vimepongeza juhudi za rais kuhakikisha mchakato wa katiba unakwenda mbele ukihusisha wadau wote na wale walioachwa wasikilizwe kwa lengo la kuwaleta pamoja.
Mbatia alisema vyama vyao vinampongeza Rais Kikwete kwa nasaha zake kwa njia ya mazungumzo wakisema ni sahihi na ahadi ya kutoa ushirikiano mkubwa katika kila hatua ya mchakato wa katiba akiwa na lengo la kuona katiba inakuwa ya wote.
Kwa mujibu wa tamko hilo la TCD mkutano huo wa Ikulu na vyama sita vyenye wabunge na rais vilikubaliana kushirikisha vyama vingine 15 visivyo na wabunge kuandaa mapendekezo ya kina ya upungufu wa muswada ambao sasa umekuwa sheria na kupendekeza marekebisho maalumu na kuyawasilisha haraka iwezekanavyo.
Vile vile walipendekeza kuwa baada ya kuwasilisha mapendekezo hayo serikalini ili serikali iunde kamati maalumu ya kukutana na vyama hivyo kujadili kwa kina juu ya upungufu katika sheria husika na kukubaliana juu ya maeneo muhimu yanayohitaji marekebisho kwa lengo la kuufanya mchakato wa katiba kuwa shirikishi.
Mbatia alisema kulingana na makubaliano waliyofanya na rais, baada ya pande zote kukutana serikali itaandaa hati ya dharura ili sheria husika irejeshwe bungeni haraka katika mkutano wa Bunge unaoanza wiki ijayo.
Alisema kuwa katika mjadala wa kitaifa, taasisi mbalimbali katika umma, makundi ya kijamii na wadau wote muhimu wahusishwe ili kutengeneza maridhiano ya kitaifa.
Mbatia alitoa wito kwa niaba ya vyama vyote vya siasa kuwaomba Watanzania wote hususani wabunge waunge mkono juhudi hizo za vyama na Rais Kikwete kuhakikisha mchakato wa katiba mpya unakuwa shirikishi utakaolinda maslahi mapana ya taifa.
Tamko hilo lililosomwa na Mbatia lilikuwa limesainiwa na Philip Mangula (CCM), Freeman Mbowe ambaye aliwakilishwa na Dk. Slaa (CHADEMA), Prof. Ibrahim Lipumba (CUF), James Mbatia (NCCR-Mageuzi, Augustino Mrema aliyewakilishwa na Nancy Karia (TLP), John Cheyo aliyewakilishwa na Isaac Cheyo (UDP) na Fahmi Dovutwa wa UPDP kwa niaba ya vyama visivyo na wabunge.
Mangula agoma kuisema CCM
Baada ya tamko hilo, wakati wa maswali, waandishi walitaka kujua kauli ya CCM kwani wamekuwa wakisisitiza kuwa mchakato huo ulikuwa huru na ulipitia hatua zote, kama wapo tayari kufanya mabadiliko kama alivyopendekeza rais na vyama vyenye wabunge.
Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Philip Mangula aligoma kuzungumza kwa undani na kusema: “Mimi sio mbunge siwezi kuwasemea wabunge.”
Kauli hiyo ilisababisha Mbatia kuanza upya kuwataka waandishi na Watanzania waache tofauti zao, waache kauli zote zilizowahi kutolewa na kutoa fursa mpya ya kuanza mchakato kwa njia ya amani kwa maslahi mapana ya taifa.
Chanzo – Tazania daima