Monday, 21 March 2011

KIKUNDI CHA TAARAB CHA FIVE STAR MODERN CHAPATA AJALI MBAYA USIKU HUU NA WATU ZAIDI YA KUMI WAHOFIWA KUFA







Muimbaji Issa Kijoti ni miongoni mwa  waliofariki dunia katika ajali hiyo


Habari za kuaminika  tulizopata usiku huu kutokea Mkoa wa Pwani kuwa kikundi cha Taraab cha Five Stars Modern kimepata ajali mbaya kikiwa kinatokea Songea Mkoa wa Ruvuma kuelekea jijini Dar kwa shuhuli zake za Taarab
Ajali hiyo imetokea Mikumi -Morogoro ambapo Bus lao la abiria la Toyota Coaster kuligonga lori lililokuwa limeharibika  limeegeshwa bara barani na kupinduka inasemekana watu wanane wamekufa hapo hapo na wengine wawili wamekufa njiani kuelekea Hospitali ya Tumbi iliyopo Kibaha Mkoa wa Pwani na wengine wameumia na hali zao ni mbaya sana  Bus hilo lilokuwa limepakia wanamuziki   22  Habari zaidi tutawaletea baadae


 

No comments:

Post a Comment