Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa imekutana jana tarehe10/06/2013 chini ya uenyekiti wa Mwenyekiti wa Taifa wa CCM Dr. JakayaMrisho Kikwete. Kikao hicho kilikuwa cha siku moja na maalum kwa ajili yakupokea rasimu ya katiba mpya.
Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa imekutana jana tarehe 10/06/2013 chini ya uenyekiti waMwenyekiti wa Taifa wa CCM Dr. Jakaya Mrisho Kikwete.
Kikao hicho kilikuwa cha siku moja na maalumkwa ajili ya kupokea rasimu ya katiba mpya.Kamati Kuu inaipongeza Tume ya Mabadiliko ya Katiba nchini kwa kazi nzuri na kukamilisha kazi kwawakati.Kamati Kuu imepokea rasimu hiyo na kuelekeza kuwa;Kwa kuwa rasimu hii ni ya kwanza ambayo inapelekwa kujadiliwa tena kwa wananchi kupitia mabarazambalimbali ya katiba baada ya kuisha kwa hatua ya kutoa maoni.Kamati Kuu imekiagiza Chama kijipange kuijadili rasimu hiyo ndani ya Chama kama baraza la kitaasisi lakatiba na kuwataka wanachama na wapenzi wa CCM wajitokeze kwa wingi na kushiriki kwenyemabaraza haya.Ushiriki huu wa CCM baada ya kupokea rasimu umekusudia kushirikisha wanachama wetu kwenye ngaziya tawi, wilaya, mkoa na Taifa.Lakini pia Jumuiya za CCM zimekusudia kushiriki kama mabaraza ya Katiba na hivyo kuongeza ushirikiwa wanachama na wapenzi wa CCM katika mchakato huu.CCM kama baraza la katiba la kitaasisi litaipitia rasimu iliyowasilishwa kifungu kwa kifungu na kwakuzingatia maoni ya CCM yaliyotolewa mwanzoni kabisa mwa mchakato wa mabadiliko ya Katiba,wanachama wetu watashiriki kutoa maoni yao.Pamoja na kazi nzuri ya Tume ya Mabadiliko ya katiba, Kamati Kuu inaiomba Tume hiyo kueleza vizurimchakato mzima kutoka rasimu ya kwanza mpaka rasimu ya mwisho ili kuondoa mkanganyiko kwawananchi juu ya mchakato mzima hasa baada ya rasimu ya kwanza kutoka.Kamati Kuu inawasihi Watanzania kushiriki tena kwenye kutoa maoni kupitia mabaraza ya katiba kwarasimu ya kwanza, bunge maalum la katiba kwa rasimu ya pili na kupitia kura ya maoni kwa rasimu yatatu, kwa amani,utulivu na kuvumiliana ili mwisho wa siku tupate Katiba nzuri ya nchi yetu kwa masilahiya Watanzania walio wengi.
Nape Moses Nnauye
CCM Secretary for Ideology & Publicity















No comments:
Post a Comment