
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akikabidhi bendera ya Zanzibar kwa watoto mayatima na viongozi wao wanaokwenda nchini Uturuki kuiwakilisha Zanzibar katika kongamano la kimataifa kuhusu siku ya watoto yatima litakalofanyika mjini Istambul Uturuki kuanzia tarehe 28/05 hadi 03/06/2012
Watoto hao Salum Ali Mohd (miaka 10), Hajir Khalid Haji (miaka 11), Shufaa Mohd Ali (miaka 12) na Lutfia Sheha Mussa (miaka 11) wataongozana na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Muzdalifat Sheikh Abdalla Hadhir, Katibu wa Jumuiya ustadh Farouq Hamad Khamis na Mkuu wa kitengo cha mayatima Zanzibar Nassra Suleiman Abdallah.
Mapema Maalim Seif aliwakabidhi watoto hao bendera ya Zanzibar na kuwataka kuiwakilishi vyema nchi yao. Watoto hao na viongozi wao wanatarajiwa kuondoka nchini tarehe 28 mwezi huu.
No comments:
Post a Comment